Professional Documents
Culture Documents
4/5/2016
First National Bank yafungua tawi Mwanza
Benki ya First National Bank Tanzania (FNB) imeendelea kupanua wigo kitaifa
kwa kufungua tawi jipya eneo la Rock City Mall jijini Mwanza leo.
Akizungumza wakati wa ufunguzi, Mkuu wa Biashara wa benki hiyo, Francois
Botha alisema uzinduzi wa tawi la FNB Mwanza umelenga kukidhi ongezeko
kubwa la mahitaji ya huduma za kibenki na za kifedha katika mkoa huo.
Uzinduzi wa tawi la Mwanza ni sehemu ya uwekezaji endelevu na mkakati
wa kuhakikisha maeneo mengi ya nchi yanapata huduma bora za kifedha.
Pia tumezingatia ukuaji wa haraka wa mkoa wa Mwanzaambao una mchango
mkubwa katika kukuza uchumi wa Tanzania.
Botha alisema tawi Mwanza ni la tisa miongoni mwa mtandao wa matawi ya
FNB Tanzania ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa kupanua mtandao wa
matawi ili kuyafikia maeneo yote nchini.
First National Bank daima tunafikiri njia mbalimbali za ambazo tunaweza
kutoa huduma za kibenki kwa urahisi kwa wateja wetu. Tawi letu la Mwanza
litatoa ufumbuzi wa kina kwa wateja wanao ishi Mwanza na maeneo jirani
yenye biashara inayokua kwa kasi Botha alisema.
Mara kwa mara tunafikiria mbinu mpya za kutuwezesha kutoa huduma
inayowapa unafuu wateja wetu kwa kupeleka huduma hiyo karibu na makazi
pamoja na biashara zao. Tawi hili litarahisisha huduma kwa wateja wetu
wanaoishi jijini Mwanza na maeneo ya jirani ambayo yana biashara nyingi
zinazokua kwa kasi, alisema Botha.